Tafuta katika Blogu Hii

Jumatano, 15 Aprili 2015

ZIJUE TIBA ZA MIMEA INAYOTUZUNGUKA



ALOVERA(LITEMBWE)




Alovera ni mmea wenye uwezo wa kutibu magonjwa mengi kama vile;
1.Malaria
2.Kisukari
3.Saratani
4.Mkanda wa jeshi
5.Vidonda tumbo
6.Baridi yabisi
7.Maumivu ya viungo
8.Homa ya matumbo
9.Mwili kuvimba
10.L/B/P
11.Madhara ya ukiumwa na wadudu
12.Bawasiri
13.Kuinua CD 4
14.Nguvu za kiume
15.Kuchelewa hedhi
16.Kurefusha maisha kwa wale wenye VVU
17.Hamu ya kula
18.Husaidia kuyeyusha chakula
19.Mkojo utokao kwa shida
20.Pumu
21.Ini
22.Figo
23.Ngozi na masikio kutoa usaha

Matayarisho ;Hutegemea aina ya ugonjwa unaotaka kuutibu



TANGAWIZI;
 Tangawizi ijapokuwa ni kiungo katika vyakula pia ni dawa yenye uwezo wa kutibu maradhi mbalimbali yanayomsibu binadamu.Baadhi ya maradhi hayo ni;
1.Tumbo-hutuliza maumivu ya tumbo yanayotokana na matatizo ya usagaji wa chakula
               -kuharisha,kuvimbiwa.(Inapotumiwa katika chakula husaidia usagaji wa chakula na inaleta hamu ya kula)
2.Kichefuchefu na kutapika-Huondoa kichefuchefu
3.Matatizo ya moyo-Huimarisha moyo na kumuepusha mtu maradhi ya moyo
4.Matatizo ya kupumua-Inapunguza kiwango cha mafuta mwilini
   -Huondoa homa ya mafua
   -Hutibu pumu
5.Maumivu-Maumivu ya misuli
                  -Maumivu ya kichwa,shinikizo la damu,mawazo,kizunguzungu na kukosa umakini
6.Maumivu wakati wa hedhi
7.Husaidia kutibu malaria na homa ya manjano
8.Nguvu za kiume na kuboresha manii
9.Vijiwe katika figo
10.Hufaa kutunzia nywele kwani huondoa uyabisi
11.Husaidia katika tiba ya saratani na kuzuia saratani
12.Husaidia kwa wenye kufunga hedhi na kusaidia kutoka


  NAZI;
Nazi ina Vitamin A,B na E
Baadhi ya faida za nazi ni;
a.Huimarisha utumbo
b.Upungufu wa damu
c.Husaidia mapafu
d.Huondoa uchovu wa mishipa pamoja na magonjwa ya mishipa
e.Kuondoa uchovu mwilini
f.Huondoa usahaulifu
g.Huimarisha viungo
h.Homa

MATUMIZI;Jinsi ya kutumia wasiliana na LMTM HERBAL CENTER
MOBL;+255776 217417
fax2email+255736601119
email;lmtmherbal@rocketmail.com

JE WAJUA KABICHI NI DAWA?




Kabichi ni zao  linalolimwa mahala pengi sana hapa duniani.Mara nyingi mboga hii imekuwa ikichukuliwa kama ni aina fulani inayotakiwa kuliwa na watu wa chini au kutumika katika kachumbari tu.Huwa inatumika zaidi sehemu za jumuiya kama vile shule,magerezani na vyuoni kwani gharama yake ni ndogo hivyo mnunuzi anaweza kuhimili kuinunua kwa matumizi ya watu wengi.Mboga hii ina manufaa mengi sana mwilini lakini iwe ya rangi ya kijani,nyekundu au hata zambarau na sio ile iliyokaa sana sokoni hadi kusinyaa,hiyo haina manufaa kabisa kwa mwili wa binadamu.

FAIDA ZA KABICHI;
1.Huzuia saratani-Ulaji wa kabichi huzuia saratani ya matiti,utumbo mpana na saratani ya korodani(testes)kwa wanaume.Kwani ina madini yanayosaidia kupigana na visababishi vya saratani.Pia huzuia uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo.
Mboga hii huondoa lehemu (cholesterol)katika damu,kwani huleta shinikizo kubwa la damu pale yanapojaa,pia huweza kusababisha kiharusi na moyo kupasuka.Hivyo kabichi husaidia kuondoa.
2.Kuondoa sumu mwilini-Kabichi ina Vitamin C kwa wingi kuliko hata machungwa,pia ina kampaundi za sifa,vitu hivi huisaidia sana kusafisha damu na kuondoa sumu mwilini.Pia huimarisha ini hivyo kulifanya lifanye kazi vizuri.
3.Ina Vitamin kwa wingi-Kabichi ina Vitamin A,B,C,E na K kwa wingi ambazo zina faida kubwa sana mwilini kama;
a.Vitamin A huisaidia kuimarisha ngozi na uwezo wa kuona.
b.Vitamin B huimarisha uwezo wa kutafakari na kuboresha utendaji wa kazi wa ubongo na kuzuia msongo wa mawazo.
c.Vitamin C huimarisha kinga ya mwili na kuzuia visababishi vya saratani
d.Vitamin E hufanya ngozi ya mwili kuwa nyororo
e.Vitamin K huimarisha mifupa na uhusika na ugandaji wa damu pale unapoumia.
Manufaa mengine ni kama vile kulinda mwili na maambukizi ya magonjwa mbalimbali,pia hutibu vidonda vya tumbo,kwani utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha tiba cha Stanford,iligundulika kuwa wagonjwa 13 walipona vidonda vya tumbo kwa kunywa juisi ya kabichi.Pia hupunguza tatizo la kufunga choo kwani ina kambakamba zinazosaidia kulainisha choo na vilevile ina madini ya salfa na chuma yanayosaidia kusafisha utumbo.
    JINSI YA KUANDAA KABICHI;
 Kabichi inapendekezwa sana kuliwa ikiwa mbichi kwa kuongezwa ndimu na chumvi ili kuleta ladha nzuri kama vile kachumbari,vilevile unaweza tu ukaichemsha supu yake lakini isiive sana kiasi cha kuua virutubisho vyake,inapendekezwakuchemka kwa dakika 4-5 tu.
  ANGALIZO;Ulaji wa kabichi uliopitiliza huweza kusababisha ugonjwa wa Rovu(goiter)kwa hiyo watu wenye tatizo la rovu wasile kabichi kwa wingi.

KWA MAWASILIANO NA MAELEKEZO ZAIDI YA JINSI YA KUTUMIA KULINGANA NA TATIZO UTAKALOKUWA NALO WASILIANA NA OFISI ZETU KUPITIA;
MOBL;+255776217417,
fax2email+255736601119
email;lmtmherbal@rocketmail.com

Jumatatu, 12 Januari 2015

PROSTATITIS(TATIZO LA KIBOFU CHA MKOJO)





Tatizo hili watu wengi hulifahamu kama kibofu cha mkojo.PROSTATE-Ni kikokwa kidogo kilichopo chini ya kibofu cha mkojo.Kazi ya prostate ni kutoa majimaji kama maziwa ambayo kazi yake kubwa ni kubeba na kusafirisha mbegu za kiume kupitia njia ya mkojo(urethra)na kwenda kunakohitajika.
Jinsi umri wa mwanaume unavyosonga mbele PROSTATE huongezeka ukubwa(kuvimba).Hali hii husababishwa aidha na upungufu wa LYCOPENE(ambayo hupatikana kwa wingi kwenye nyanya)au maambukizi (infection)au sababu nyinginezo kama maambukizi ya vijidudu (FUNGI).Kuvimba kwa prostate husababisha kugandamiza kwa kibofu cha mkojo kiasi kwamba mkojo kidogo ukiwa ndani ya kibofu mtu hudhani kibofu kimejaa kumbe sio.
DALILI ZA MTU MWENYE PROSTATE NI;
1.Kubanwa na mkojo mara kwa mara
2.Kwenda haja ndogo mara kwa mara usiku
3.Damu kwenye mkojo au kwenye mbegu za kiume
4.Maumivu wakati wa kukojoa
5.Maumivu baada ya kukojoa au wakati mtu anamaliza kukojoa
6.Kushindwa kukojoa
7Maumivu wakati mbegu za kiume zinatoka
8.Maumivu kwenye hipsi,mgongo,nyonga au mapajani
9.Matone ya mkojo kutoka yenyewe au kushindwa kujizuia na kukuta mkojo umetoka
-Mtu mwenye tatizo hili anaweza kujihisi kama amepungukiwa nguvu za kiume(sprerm count)kitu ambacho kwa kiasi kikubwa sio kweli.Hali hii husababishwa na ile hali ya yale majimaji yanayosafirisha mbegu za kiume kutokuwepo kwa kuishia njiani.Hali ikizidi kuwa mbaya huweza kusababisha muathirika kufanyiwa upasuaji kwaajili ya kuondoa prostate hiyo au kusababisha mtu kupata saratani(PROSTATE CANCER)
USHAURI;Wanaume wanashauriwa kuwa na mazoea ya kula nyanya kwa wingi(iliwe bila kupikwa au kuongezewa kitu chochote kama chumvi),papai,zabibu na mapera kama kinga.ukiweza kula nyanya kwa wingi kila siku itakuwa ni vizuri zaidi.
 Hata hivyo habari nzuri ni kuwa katika kituo chetu cha LMTM HERBAL CENTRE tunazo dawa ya LMTM-RUN/4.5.1 na LMTM/S32/J zenye uwezo mkubwa wa kutibu tatizo hili likiwa bado katika hatua za awali.

KWA MASWALI,USHAURI NA TIBA;
MOBL;+255798353434
fax2email+255736601119
email;lmtmherbal@rocketmail.com

Jumapili, 7 Desemba 2014

UFAHAMU UGONJWA WA ZINAA WA CHLAMIDIA,DALILI ZAKE ,MADHARA,TIBA NA KINGA


Chlamidia ni aina ya ugonjwa ulio katika kundi la magonjwa ya zinaa(STD) unaosababishwa na bacteria aina ya CHLAMIDIA TRACHOMATIS,ambao wanaweza kuathiri viungo vya uzazi na pia kusababisha ugonjwa wa homa ya mapafu unaojulikana kama TYPICAL PNEUMONIA.Kati ya magonjwa ya zinaa yanayosababishwa na bakteria,chlamidia ndio ugonjwa unaoongoza kwa maambukizi duniani ambapo nchini Marekani pekee inakisiwa watu milioni 4 huambukizwa ugonjwa huu kila mwaka.
  Inawezekana jina la ugonjwa huo halijazoeleka katika masikio ya wengi na hii huenda ni kutokana na kutokuwepo kwa takwimu za kutosha kuhusiana na suala hilo katika nchi nyingi barani Afrika na hasa katika nchi zetu za Afrika Mashariki,hivyo ni vigumu kujua idadi kamili ya maambukizi.Lakini bila shaka chlamidia ndio ugonjwa wa zinaa unaotokana na bakteria unaoongoza kwa maambukizi mengi zaidi duniani ukifuatiwa na ugonjwa wa gono.Gonjwa hili ambalo huwaathiri wanawake na wanaume pia linaweza kuleta madhara makubwa ikiwa ni pamoja na kuharibu mfumo wa uzazi wa mwanamke.
  Nchini Marekani pekee mwaka 2011 kesi milioni 1 na nusu ziliripotiwa katika hospitali katika majimbo 50 ya nchi hiyo,katika hali ambayo kesi nyingi hazikuripotiwa kwa kuwa watu wengi wenye kuambukiza ugonjwa huo huwa hawaonyeshi dalili na hivyo hawakwenda hospitali.Kama yalivyo magonjwa mengi ya zinaa,chlamidia pia huwapata zaidi vijana na takwimu zinaonyesha kuwa kati ya wasichana walio na umri wa miaka 14-15 wenye kufanya ngono zembe mara kwa mara,mmoja wao huambukizwa chlamidia.
   Ugonjwa wa chlamidia huweza kuambukizwa kupitia njia za kujamiiana .Mtu yoyote mwenye kufanya ngono zembe na mtu aliye na ugonjwa huo anaweza kuambukizwa.Pia mama mjamzito huweza kuambukiza mtoto wake wakati wa ujauzito.Vilevile ugonjwa huo wa zinaa unaweza kuambukizwa kupitia mbwa,vinyesi vya wanyama kama vile ndege walioambukizwa aina ya chlamidia inayopatikana kwa wanyama kwa mfano kuku,bata,kasuku na kadhalika na kusababisha aina ya homa ya mapafu inayojulikana kama PSITTACOSIS ambayo huambatana na homa kali yenye nyuzi joto kati ya celsius 39.4 hadi 41.1.Chlamidia huathiri sehemu tofauti za mwili wa binadamu kama macho,mfumo mzima wa kupumua,sehemu za siri,viungo vya uzazi na tezi(lymph nodes)

     DALILI NA VIASHIRIA VYA UGONJWA WA CHLAMIDIA
 -Asilimia 75 ya wanawake na asilimia 50 ya wanaume wanaopata maambukizi ya ugonjwa huu huwa hawaonywshi dalili zozote za ugonjwa huo ila dalili hutokea baada ya wiki 1-3 baada ya mtu kupata maambukizi.

   DALILI KWA WANAWAKE;
1)Kutokwa na majimaji ya rangi ya njano yanayotoka kwenye utupu,ambayo huwa na harufu kali
2)Kuhisi maumivu wakati wa haja ndogo
3)Kuhisi kama kuwaka moto wakati wa kukojoa
4)Kutokwa na damu katikati ya kipindi cha hedhi yaani baada ya kumaliza mzunguko wa hedhi na kabla ya kuanza mzunguko mwengine
5)Kuhisi maumivu sehemu ya chini ya tumbo
6)Kuhisi maumivu wakati wa kujamiiana
7)Kutokwa na damu wakati wa kujamiiana na pia kuvimba na kuhisi maumivu kwenye tezi zilizopo sehemu za siri

   DALILI KWA WANAUME;
1.Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
2.Kuhisi kama kuwaka moto wakati wa kukojoa,
3.Kutokwa na njimajikwenye uume ambayo yanaweza kuwa ya ragi nyeupe kama maziwa,kijivu au rangi ya njano.
4.Sehemu ya tundu kwenye uume kuwa nyekundu,kuvimba na kuwasha.
5.Kuhisi maumivu kwenye korodan na tezi zilizopo sehemu za siri ambazo huvimba na huambatana na maumivu.Mara nyingi dalili hizi kwa wanaume huja na kupotea au zinaweza kuonekana tu wakati anapoenda kukojoa asubuhi baada ya kuamka kutoka usingizini.
-Dalili za ugonjwa huu kama umeathiri puru(rectum) kwa wanawake na wanaume ni kama ifuatavyo;
     a)Kuwashwa na kutokwa na damu kwenye puru
     b)Maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa
     c)Kutokwa na uchafu kama kamasi kwenye puru(rectum)
Iwapo vimelea vya chlamidia vitaathiri macho,wanawake na wanaume huwa na dalili zifuatazo;
 -Uvimbe kwenye macho
 -Macho kuwa mekundu
 -macho kuwasha na hata kutokwa na majimaji machoni.
Baada ya mtu kuhisi dalili hizo tulizozitaja ,hupaswa kwenda hospitalini au katika kituo cha afya ili kupimwa na kuthibitishwa kwamba ana ugonjwa huo ili apatiwe matibabu.
  Vipimo vya uchunguzi vya ugonjwa wa chlamidia ni Urethral swab for culture.Katika kipimo hiki majimaji kutoka kwenye uume au uke huchukuliwa kwa kutumia kijiti chenye pamba au swab maalum ambayo hupelekwa maabara ili kuoteshwa na kuangalia aina ya uoto wa bakteria.Pia huchukuliwa vipimo vya mkojo na pia kipimo cha PCR au Polymerase Chain Reaction,ambacho ni cha kuangalia vinasaba vya bakteria au DNA na hufanywa katika maabara.Baada ya majibu kuonyesha kuwa mgonjwa ameambukizwa vimelea vya ugonjwa huo matibabu hufuata.Chlamidia ni kati ya magonjwa ya zinaa yanayotibika na ugonjwa huu hutibiwa kwa dawa aina ya antibiotiki zilizopo kwenye makundi ya macrolides,Quinolones na Polyketides ambazo hutolewa chini ya maelekezo ya daktari.

 MADHARA YA UGONJWA WA CHLAMIDIA;
  Kwa wanaume;
-Huathiri korodani na kusababisha mwanaume kukosa uwezo wa kuwa na watoto au kuwa tasa na pia husababisha maambukizi kwenye tezi dume(prostates).
Kwa wanawake;
-Husababisha maambukizi kwenye mirija ya uzazi,mfuko wa uzazi na mayai ya uzazi,kwahivyo kusababisha ugonjwa wa uvimbe katika fupanyonga au Pelvic inflammatory disease(PID).Pia huongeza uwezekano wa wanawake kupata mimba zilizotunga nje ya mfuko wa uzazi ambazo kitaalam huitwa Ectopic pregnancy.Mbali na hilo,mwanamke hupata maumivu sugu kwenye nyonga na ugonjwa wa mifupa arthritis aina ya Reiters syndrome.
-Vilevile chlamidia huweza kusababisha ugumba kwa mwanamke kama hatapata tiba.Si hayo tu,kwa wanawake wajawazito chlamidia husababisha wajifungue kabla ya wakati wake.Pia mtoto anaweza kuzaliwa na maambukizi kwenye masikio,sehemu za siri,macho,mapafu (homa ya mapafu),na kama mtoto hatopatiwa tiba ya haraka ya macho baada ya kuzaliwa basi anaweza kuwa kipofu.
-Dalili za chlamidia kwa watoto wachanga hutokea katika kipindi cha wiki 2 kwenye macho,na iwapo ni homa ya mapafu dalili zake hujitokeza katika kipindi cha wiki 2-miezi 3 baada ya kuzaliwa.

  NJIA ZA KUJIKINGA NA UGONJWA WA CHLAMIDIA;
-Kwa wanawake wajawazito,ni vizuri kuhudhuria klinik mapema wakati wa ujauzito na kupima vipimo mbalimbali ambapo kimojawapo ni cha kuangalia iwapo mama mjamzito ameathirika na ugonjwa huu ili aweze kupatiwa matibabu mapema
-Kwa wenye maambukizi wanashauriwa kuchukua tahadhari ya kutowaambukiza wapenzi wao kwa kufanya ngono salama,pia kuepuka kushika macho kwa kutumia mikono na hata ikiwezekana kuwaepuka wapenzi wao ili kuwalinda na maambukizi.
-kwa  wale ambao wapenzi wao wameambukizwa au wameonyesha dalili za ugonjwa huu,wanashauriwa na wao pia kupata tiba hata kama hawana dalili zozote pia kondom zihusike kwa kila tendo la ndoa.

NB;Njia kuu na sahihi ya kujikinga na magonjwa ya zinaa ni kuacha au kuepuka kujamiiana au kufanya ngono zembe na zisizo salama.

MOBL;+255776 217 417
fax2email+255 736 601119
email;lmtmherbal@rocketmail.com

Ijumaa, 3 Oktoba 2014

JE WAJUA KUWA VYOMBO VYA PLASTIKI NI MOJAWAPO YA VYANZO VYA SARATANI ?SOMA HAPA






-   Kwa mujibu wajumuia ya madaktari wa marekani baadhi ya vyanzo vya saratani ni vifaa vya plastiki.Plastiki ikipatajoto inatoa kemikali inayoweza kusababisha aina 52 za saratani.
 -  Ili kupunguza uwezekano huo unashauriwa
(1)Usinywe chai kwa kutumia vikombe vya plastiki
(2)Usile chochote chenye moto kilichofungwa ndani ya mfuko wa plastiki kama chips nk.
(3)Usipashe chakula ndani ya microwave kwa kutumia chombo cha plastiki
(4)Epuka kuchoma mabaki ya plastiki sehemu wanakoishi watu kwani ukivuta moshi huo  ni hatari na pia inaweza kusababisha saratani ya mapafu nk




 NB;  TAFADHALI CHUKUA TAHADHARI
   SHARE KWA KUWAJULISHA WENGINE
     USISAHAU KULIKE PAGE YETU

Jumamosi, 20 Septemba 2014

UFAHAMU UGONJWA WA ZINAA WA TRICHOMONIASIS AMBAO HUWAATHIRI SANA WANAWAKE






Ugonjwa wa Trichomoniasis ni mojawapo ya ugonjwa ulio katika kundi la magonjwa ya zinaa zaidi ya 25 yanayofahamika kwa watu wengi.Ugonjwa huu huwaathiri sana wanawake kuliko wanaume.Ugonjwa huu wa Trichomoniasis unasababishwa na vimelea vya jamii ya protozoa vinavyojulikana kama Trichomonas Vaginalis ambao huathiri mrija wa kupitishia mkojo(urethra)na tupu ya mwanamke.Trichomoniasis pia hujulikana kwa majina mengine kama Trichomonas Vaginitis au Trich.
Ugonjwa huu huathiri watu milioni 170 kwa mwaka duniani kote .Nchini Marekani pekee ambayo imeendelea katika fani ya tiba watu milioni 8 huambukizwa ugonjwa huu.Ugonjwa huu huonekana sana kwa wanawake kuliko wanaume kutokana na wanaume kutoonyesha dalili zozote wakati wa maambukizi au kutokana na majimaji ya kwenye tezi dume kuwa na madini ya Zinc ambayo huathiri vimelea hivi vya Trichomonas Vaginalis vinavyosababisha ugonjwa huo.

MAAMBUKIZI;
Trichomoniasis huambukizwa kwa njia ya kujamiiana bila kutumia kinga na mtu aliyeathiriwa na ugonjwa huo.Wanawake wengi wamekuwa wakisumbuliwa na ugonjwa huu ,ili kuufahamu ugonjwa huu vyema kwanza tufafamu nini kinachotokea wakati wa maambukizi(PATHOFIZIOLOJIA)ya ugonjwa huu.
-Umbile la vimelea vya Trichomonas Vaginalis ni sawa na chembechembe moja ya damu nyeupe  kwa upana ingawa wakati mwingine ukubwa unaweza kutofautiana kulingana na mazingira.
-Kuwepo kwa umbile kama mikono kwa nje ya kwenye kimelea hicho inayojulikana kama FLAGELLUM ,husaidia vimelea hivi kuingia kwenye tishu za mrija wa kupitishia mkojo na tupu ya mwanamke na hivyo kuharibu seli aina ya EPITHELIUM na kusababisha vidonda katika tishu hizo hali ambayo husababisha watu walioathirika na ugonjwa huu kuwa kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa VVU na magonjwa mengine ya zinaa.
Trichomoniasis huanza kuonekana kuanzia siku ya 4-28 baada ya mtu kupata maambukizi.Kwa wanawake Trichomoniasis huathiri shingo ya kizazi (cervix),mrija wa mkojo,tupu ya mwanamke,kibofu cha mkojo na tezi zinazojulikana kama BARTHOLIN Glands na Skene Glands.
-Kwa wanaume vimelea hivi hupatikana katika sehemu za siri,sehemu ya nje ya mrija wa kupitishia mkojo(Anterior Urethra),kwenye tezi dume,kwenye mirija ya kuhifadhi na kutoa mbegu za kiume(EPIDIDYMIS) na hata kwenye mbegu zenyewe.

DALILI KWA WANAWAKE;
1.Uchafu unaotoka kwenye tupu ya mwanamke ambao huwa na rangi mchanganyiko ya njano na kijani au rangi kama kijivu na huwa mzito sana.
2.Maumivu wakati wa tendo la ndoa
3.Kutoka harufu kwenye tupu ya mwanamke
4.Maumivu wakati wa kujisaidia haja ndogo
5.Shingo ya kizazi kuwa nyekundu hali ambayo hugundulika wakati daktari anamfanyia mgonjwa uchunguzi
6.Kuwashwa sehemu za siri(sio wanawake wote)
7.Maumivu chini ya kitovu kwa baadhi ya wanawake
Ingawa wanawake ndio huonyesha dalili na viashiria vya ugonjwa huu mara nyingine wanaweza kuwa na vimelea hivi hata kwa muda wa miaka kadhaa hata kama vipimo vya uchunguzi havitaonyesha kama wameathirika na vimelea vya ugonjwa huu.

DALILI KWA WANAUME;
Baadhi ya wanaume huwa hawaonyeshi dalili zozote .Baadhi ya dalili zinazoonekana ni;
1.Kuwashwa ndani ya uume
2.Kutokwa na uchafu au majimaji kwenye uume
3.Kuwashwa au kuhisi kichomi baada ya kujisaidia haja ndogo au baada ya kutoa mbegu za kiume
Baada ya mtu kuhisi dalili hizo anashauriwa kwenda hospitali au katika vituo vya afya ili kufanyiwa uchunguzi na vipimo.
VIPIMO;
Trichomoniasis hugundulika kwa kutumia vipimo
1.Kipimo cha darubini ambapo daktari humfanyia mgonjwa uchunguzi kwa kuingiza kifaa maalum katika tupu ya mwanamke na kuchukua kipimo kwa kutumia pamba maalum.Hatua hii hufanywa kitaalam bila kusababisha maumivu kwa mgonjwa na kisha kupelekwa maabara ili kuangalia kama kuna vimelea vya Trichomonas Vaginalis.Kwa kufanya uchunguzi huu daktari anaweza pia kuangalia kama kuta za ndani za tupu ya mwanamke au shingo ya kizazi (cervix) zimeathirika kwa kuwa na vidonda ambavyo ni vyekundu.
2.Kwa mwanaume daktari huchukua kipimo cha uchafu unaotoka sehemu za siri au hupangusa sehemu hizo za siri za mwanaume kwa wale ambao hawatoi uchafu au majimaji yoyote kwa kutumia pamba na kupeleka maabara kufanyia uchunguzi.Pia kipimo kilichochukuliwa na daktari kinaweza kuoteshwa kwenye maabara(culture) na kuangalia kama kuna uoto wa vimelea vya Trichomonas Vaginalis baada ya siku tatu.
3.Kuangalia kiwango cha tindikali(PH)-daktari anaweza kuangalia kiwango cha tindikali kwenye tupu ya mwanamke kwa kutumia karatasi maalum ya kkipimo hiki ijulikanayo kama PH paper,ambapo kiwango kama ameathirika itakuwa PH zaidi ya 5.Kwa kawaida PH ya tupu ya mwanamke inakuwa ni ya tindikali(acidic) kuanzia PH 3.8-4.5 .Magonjwa yanayobadilisha PH ni pamoja na;Trichomoniasis na Bacteria Vaginosis.Mabadiliko hayo humfanya mwanamke kuwa kwenye hatari ya maambukizi tofauti.
4.Kipimo cha damu -hufanywa ili kuchunguza Prostate Specific Antigen(PSA).PSA ni aina ya protin inayozalishwa na seli za tezi dume.Uzalishaji wake huongezeka wakati seli za tezi dume zinapoongezeka kuelekea kuwa kansa inayojulikana kitaalam kama BPH au wakati tezi dume inapopata maambukizi(PROSTITIS),na katika saratani ya tezi dume.Kipimo hiki hufanywa kwa wanaume wanaopata ugonjwa wa Trichomoniasis mara kwa mara au wale wenye umri kuanzia miaka 60 na kuendelea na ambao wamepata ugonjwa huu wanapaswa kufanyiwa kipimo hiki angalau mara 1 kwa mwaka.
5.Pap smear -hiki ni kipimo kingine ambapo chembechembe au seli za shingo ya kizazi huchukuliwa na kuchunguzwa kwa kutumia darubini.Kipimo hiki pia hutumiwa katika uchunguzi wa wanawake kujua kama wamepata saratani ya shingo ya kizazi au la.Wanawake wenye zaidi ya miaka 18 au wale wenye upungufu wa kinga ya mwili wanashauriwa kufanya kipimo hiki angalau mara 1 kwa mwaka ili kujua afya zao.
6.Kipimo cha kuangalia maambukizi ya VVU-walioathirika na Trichomoniasis wanapaswa kufanyiwa kipimo cha kuangalia kama wameambukizwa ugonjwa wa HIV.
7.Kipimo cha mkojo na damu-hufanywa kuangalia wingi wa damu,chembechembe tofauti za damu na chembechembe bapa(Platelets)

MATIBABU;
Tiba ya trichomoniasis ni kutumia dawa aina ya Metronidazole au Flagyl.Dawa hii haitumiki kwa wanawake wenye ujauzito chini ya miezi 3 au wanaonyonyesha hivyo basi kabla ya kutumia dawa hii ni vyema ukamuona daktari.Kwa wale walioathirika na ugonjwa huu wa zinaa wanashauriwa kupata tiba pamoja na wenzi wao .Madhara mengine ya dawa ya Metronidazole mbali na madhara kwa wamama wajawazito na wanaonyonyesha ni pamoja na;
1.Mzio(mcharuko wa mwili)yaani allergic reaction
2.Kichefuchefu
3.Kukauka midomo
4.Kuharisha
5.Kuhisi ladha kama ya chuma mdomoni
6.Kushuka kiwango cha chembechembe nyeupe za damu(leukopenia)ambazo hutoa kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali na hivyo upungufu wake hufanya mtu awe  katika hatari ya kupata maambukizi tofauti tofauti.Mcharuko wa dawa hii mara nyingi hutokea iwapo masharti ya dawa hayakufatwa vyema au mtu anapokunywa dozi ya dawa zaidi ya alivyoelekezwa na daktari.Ni muhimu kufahamu kuwa unapohisi hali kama hizo katika matibabu yoyote inakupasa kuacha kutumia dawa zinazokudhuru na kumuona daktari haraka.
Katika kituo chetu cha LMTM HERBAL CENTRE tunazo dawa za mimea zisizi na kemikali zozote na isiyo na madhara kwa wajawazito na wanyonyeshao yenye uwezo wa kutibu siyo Trichomoniasis pekee bali magonjwa yote sugu ya zinaa kama kaswende,kisonono,klamidia,UTI n.k.Dawa hiyo inajulikana kwa jina la LMTM-N7/SUZ.Kwa wale waliofika katika kituo chetu ni mashahidi wa uwezo wa dawa hii kutibu magonjwa yote ya zinaa.
NB;LMTM HERBAL CENTRE ndicho kituo pekee ndani ya Tanzania,Afrika mashariki kati na kusini mwa Afrika chenye uwezo wa kutibu magonjwa ya zinaa sugu na uzazi.

MADHARA YA TRICHOMONIASIS;
1.Ugonjwa huu ni miongoni ya magonjwa ya zinaa ambayo huongeza hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa mengine kama HIV kama tulivyokwisha sema huko nyuma.
2.ugonjwa huu husababisha mwanamke kujifungua mtoto mwenye uzito mdogo
3.Huwaongezea wanawake hatari ya kupata saratani ya shingo ya kizazi
4.Kuongeza hatari kwa wanaume kupata saratani ya tezi dume.

 KITUO CHETU CHA LMTM HERBAL CENTRE KINAPATIKANA ILALA MCHIKICHINI MTAA WA USANGU,
MOBL;+255776 217 417,
fax2email+255 736 601119
email;lmtmherbal@rocketmail.com

Jumatano, 3 Septemba 2014

UNATAKA KUPUNGUZA UNENE ?SOMA HII HAPA

Hapa nakuletea ratiba ya kupunguza unene/uzito kwa muda wa siku saba kwa kutumia lishe maalum;
  (1)Siku ya kwanza asubuhi kula matunda(lakini katika matunda hayo usile ndizi).Mchana chemsha kabichi,weka chumvi kidogo na nyanya na upate supu kisha kula mchanganyiko huo.Jioni kula tikiti maji na mboga mboga au kabichi uliyotengeneza mchana.
 (2) Siku ya pili kula mboga za majani asubuhi (usile mboga za majani zenye wanga kama karoti).Mchana kula kabichi iliyochemshwa ,tengeneza na kachumbari.katika kabichi weka chumvi,pilipili na mafuta ya olive.Jioni unaweza kula mlo kama wa mchana lakini unaweza kukaanga mboga nyingine za majani.
 (3)Siku ya tatu kula mboga za majani na matunda ,unaweza kuongeza kiazi kitamu kimoja .
 (4)Siku ya nne kula ndizi moja na unywe na maziwa ya mtindi wakati wa asubuhi ,Mchana kula kabichi kama ulivyoitengeneza  kwenye siku ya kwanza,usiku rudia mlo wa mchana.
(5)Siku ya tano kula nyanya nn pamoja na samaki au kipande cha kuku asubuhi.Mchana unaweza kula samaki wa kuchemsha kiasi ambaye amechanganywa na nyanya.Wakati wa jioni unaweza kula chakula kama cha mchana.
 (6)Siku ya sita unaweza kula chakula cha protin na mboga za majani.Anza siku kwa kula kachumbari asubuhi.Mchana kula tambi kiasi na kipande kidogo cha samaki.Usiku tengeneza supu ya kabichi.
 (7)Siku ya saba anza kwa matunda na juisi,Mchana kula mboga za majani na usiku kula supu ya kabichi na kiazi kimoja.
  NB:Unatakiwa kunywa maji angalau glasi nne kila siku.Dayati hii ni kwa siku saba tu.