Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 28 Aprili 2013

JITIBU MAGONJWA MBALIMBALI KWA KUTUMIA VITU MBALIMBALI VINAVYOKUZUNGUKA


MAGONJWA NA JINSI YA KUYATIBU
(1)PUMU-
Matumizi;(a)hutibiwa kwa kutumia;simbi zaidi ya 20,ndimu nyingi na asali.Kunywa mchanganyiko huu kijiko 1 mara3 kwa siku hadi upone.AU kula vitunguu maji kwa wingi
(b)Pembe ya mbuzi-kausha kisha usage na unga wake changanya na asali na ulambe mara 3 kwa siku
(2)NGUVU ZA KIUME-
Hutibiwa kwa kutumia;
(a)kitunguu swaumu-
Matumizi;ponda na changanya na asali ya njano na ulambe asali hiyo kijiko1 mara3 kwa siku tumia mchanganyiko huu kwa wiki 2.
(b)tende na rose-
matumizi;changanya na maziwa na kisha kunywa wiki1-wiki3.
(c)mchele mkavu-
(d)Tikiti maji,tangawizi,pilipilinafaka halisi,mbogamboga za majani
Matumizi;tafuna mchele kidogo lisaa limoja kabla ya kujamiiana utarudiwa na nguvu zako.
KIFUA/KUKOHOA-
Hutibiwa kwa kutumia mchanganyiko wa;asali,kitunguu maji,kitunguu swaumu na tangawizi;
Matumizi;twanga mchanganyiko huu pamoja kisha ndio utumie.
(3)MAGONJWA YA MOYO-
Matumizi;kunywa juisi ya vitunguu maji kwa wingi.
(4)MAPAFU-
Matumizi;kula zabibu au kunywa juisi yake kwa wingi kila siku.
(5)GESI-
Matumizi;kunywa maji glasi8 au zaidi kwa siku.
(6)MAWE KATIKA KIBOFU CHA MKOJO-
Matumizi;kula chakula kilichopikwa na manjano.
(7)UVIMBE KATIKA SEHEMU ZA SIRI NYUMA-
Matumizi;paka alovera mahali penye uvimbe mara 3 kwa siku.
(8)KUPATA CHOO KIKUBWA-
Matumizi;kunyia chai ya tangawizi
(9)KICHOMI-
Matumizi;kula ndizi mbivu kila siku.
MAJIPU NA VIDONDA VISIVYOPONA-
Matumizi;binzari ya manjano koroga katika maji upate uji mzito kisha paka sehemu iliyoathirika mara2 kwa siku.AUchanganya zafarani kiasi na unga wa risasi na weka maziwa ya mbuzi kidogo kisha paka kwenye kidonda.
(10)MAUMIVU MAKALI TUMBONI-
Matumizi;changanya vijiko2 vya tangawizi na castro oil kisha kunywa mara 2 kwa siku.
(11)MIFUPA ILIYOVUNJIKA-
Matumizi;kula nusu nanasi kila siku hadi upone.AU kaanga vitunguu maji na uboho(rojorojo)
(12)MAUMIVU YA VIUNGO/MGONGO-
Vifaa;mafuta ya simsim,haba souda,na pilipili manga
Matumizi;chemsha,chuja na paka kwenye maeneo yanayouma yakiwa na uvuguvugu.
(13)KUTAPIKA DAMU-
Matumizi;weka kuzubara katika siki kali masaa24,ongeza sukari na chuja kisha unywe kutwa mara3
(14)KUSAGA CHAKULA NA KUIMARISHA TUMBO DHAIFU-
Vifaa;habasouda vijiko2, pilipili manga2,karafuu2
Matumizi;changanya kisha kunywa kijiko1 cha chai ndani ya kinywaji chochote cha uvuguvugu
(15)KIFUA/MARADHI-
Vifaa;juisi ya figili kikombe cha kahawa,kijiko kikubwa cha asali
Matumizi;changanya na maji ya moto kikombe cha chai yaache yapoe ndio unywe kutwa mara2 asubuhi na jioni.
(16)KIKOHOZI CHA MUDA MREFU-
Vifaa;khardal,asali safi ya nyuki.
(17)KUONDOA COLESTEROL-
Vifaa;tembe 3,kitunguu swaumu,kijiko1 cha zaatari,maji lita1
Matumizi;chemsha kidogo kunywa kikombe1 mara3 kwa siku.
(18)HIGH BLOOD PRESSURE/LOW BLOOD PRESSURE-
Vifaa;papai na tangawizi
Matumizi;sagapapai na tangawizi kamua juisi yake kunywa kutwa mara2 AU chemsha na kunywa juisi ya mmung'unya mara3 kwa siku
(19)KIKOJOZI-
Vifaa;ufuta mweusi na maziwa
Matumizi;saga ufuta mweusi na unga wake koroga kijiko1 ndani ya maziwa kunya mara2 kwa siku asubuhi na jioni mpaka upone
(20)HEDHI ILIYOKITHIRI/HEDHI KWA WINGI-
Matumizi;koroga unga wa ufuta mweusi ndani ya maji ya moto kisha kunywa AU chukua unga wa giligilani glasi1 chemsha katika nusu lita ya maji kisha kunywa nusu glasi mara3 kwa siku.
(21)KISUKARI-
Matumizi;chukua kijiko1 cha mdalasini weka katika kikombe cha kahawa kunywa kutwa mara3 kwa siku40 AU tengeneza juisi ya bitter gourd kunywa kila siku
(22)MAUMIVU YA MIGUU NA MAGOTI-
Matumizi;chukua kijiko1 kidogo cha zafarani changanya katika chai ya moto kunywa kutwa mara3
(23)KUZUIA MIMBA KUTOKA-
Matumizi;chukua kijiko 1 cha unga wa amla changanya na asali,kunywa kwa muda wa wiki1
(24)KUACHA SIGARA-
Matumizi;chukua hamira changanya vijiko 2 katika glasi1 ya maji na unywe pamoja na unga wake,kunywa glasi1 kutwa mara3
(25)KICHWA-
Matumizi;kula samaki na tangawizi
(26)KUVIMBIWA-
Matumizi;kula ndizi mbivu
(27)BARIDI YABISI-
Matumizi;kula tangawizi
(28)KIBOFU-
Matumizi;kula kunazi nyekundu
(29)BP-
Matumizi;zabibu nyeusi1kg,giligilani nusu,twanga kisha uchemshe na kunywa nusu glasi mara 3
(30)KWIKWI-
Matumizi;twanga hiliki changanya na maziwa kisha kunywa glasi moja
(31)DEGEDEGE-
Matumizi;ponda vitunguu swaumu kisha mpake  mwenye tatizo hilo na uichome na mfukizie
(32)UGONJWA WA KUSAHAU-
Matumizi;chukua zabibu kavu changanya na kungumanga na utafune mara2 kwa siku21
(33)MAWE KATIKA FIGO-
Matumizi;kitunguu maji chekundu,cheupe na njano,kata vipande4 kila kimoja weka vipande hivyo katika sufuria baada ya kuvisaga acha ichemke kisha kunywa jusi yake
(34)DAMU PUANI-
Vifaa;siki,limao,chumvi
matumizi;chukua chumvi kijiko kidogo weka katika glasi changanya na siki mpaka  chumvi iyeyuke ,kamulia limao nusu tumia siku3 mpaka 4 mfululizo 

TIBA MBADALA KWA KUTUMIA MBOGAMBOGA NA MATUNDA
(1)BOGA-Lina vitamini B kwa wingi
HUTIBU;
a.Huupa mwili nguvu
b.Huondoa tatizo la kufunga choo
c.Hurekebisha utolewaji wa nyongo mwilini
d.Huongeza nguvu za kiume
e.Husaidia kuvunja nguvu za sumu mwilini
f.Husaidia kupata mkojo hivyo kusafisha figo
g.Husaidia kuondoa mawe kwenye figo(Kidney stone)
h.Linafaa kwa wagonjwa wa kisukari
i.Husaidia kuimarisha glandi za kiume zitoazo mbegu za uzazi(PROSTATE GLAND
MAANDALIZI
-Chukua boga lililokomaa na katakata lisage kwenye blender(kama huna blender waweza kuliponda kwenye kinu safi na likishalainika ongeza maji kidogo kusudi upate juice yake.Wakati unakamua juice usiondoe mbegu na kiini.
NB.MAANDALIZI HAYA HUTEGEMEA UGONJWA UNAOTAKA KUUTIBU
(2)KAROTI-Ina vitamini nyingi mbalimbali
HUTIBU;
a.kulainisha tumbo
b.Inapigana na kutibu upungufu wa damu
c.Inasafisha damu
d.Inasaidia kutibu uvimbe wa saratani
e.Inatibu baridi yabisi
f.Inatibu chunusi,vidonda tumbo,koo,macho na kibofu
MAANDALIZI;
-Chukua karoti kilo1 ponda iwe laini na kisha uchemshe kwa dakika 15 ndani ya maji lita 1 na nusu au mbili chuja,kunywa juisi yake kwa kutibu vidonda tumbo au saratani ya tumbo,saratani ya kizazi tumia nusu kikombe cha chai miezi 3 mpaka 6,kwa kurembesha uso nawia juisi yake kila asubuhi mfululizo kwa siku 5.
(3)UNGA WA MKAA-
Unaweza kupata kupata kutoka kwenye mti wa mkuyu,kifuu cha nazi,msonobari au mkaratusi
INATIBU;
a.Kuumwa na nyoka
b.Kunywa sumu
c.Uvimbe
d.Kutapika,kiungulia,macho,kuharisha na kuhara damu ,kusaga chakula,vidonda tumbo,tindikali na kuungua
MAANDALIZI
a.Choma kifuu cha nazi hadi kiwe mkaa
b.Saga uwe unga(kwa miti tumia magome)
-Chukua kijiko 1 kikubwa cha unga na koroga katika maji safi ya kunywa ya vuguvugu kikombe 1 kunywa kabla ya kula kwa kutibu vidonda tumbo,kutoa asidi
KUUMWA NYOKA-
-Shona kifuko cha kitambaaa.
-Chota unga wa mkaa kijiko kikubwa na uweke ndani ya kifuko na tia maji kidogo na ufunge na nyingine ndani ya maji vuguvugu kikombe 1 uwe kama uji na umpe anywe kwa mtu aliyekunywa sumu tumia njia hiyo ya kunywa
MACHO-
-Weka katika kifuko kama hapo juu na ufunge kwenye jicho ,fanya hivyo kwa siku 3 mfululizo wakati wa usiku.
(4)GILIGILANI-
Inatibu tumbo,moyo na hedhi nk
MAANDALIZI
-Vijiko 2 vikubwa vya giligilani iliyosagwa ndani ya maji lita 1 kisha chemsha kwa dakika 10 na kunywa nusu kikombe kutwa mara 3 kwa siku 5 
(5)NYONYO-
-Majani yanatibu kifua kikuu na uvimbe wa miguu
-Mizizi ni dawa ya mafindofindo,macho ya njano,uvimbe,kisonono na kaswende
-Kikonyo chake ni dawa ya kwikwi-jaza maji ya baridi katika kikombe cha chai na kikonyo mpe mgonjwa anywe kila baada ya dakika 3 mpaka kwikwi iishe
-Kunywa punje yake na maji glasi kwa siku kwa muda wa siku 5 inatibu MOTODASI AU MOTO WA MUNGU
-Tumia majani kwa kupasha moto na kufungia miguu inayouma au kukandia miguu inayouma
-Kwa magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende mizizi kiasi na chemsha ndani ya maji nusu lita kisha kunywa kikombe cha chai kutwa mara 3 kwa muda wa siku 5
(6)SWAUMU-
HUTIBU
a.Kuumwa kichwa
b.Kibofu cha mkojo
c.Matatizo katika damu,chunusi nk
d.Macho kutoona vizuri,pumu,figo,ukurutu(fungus),baridi yabisi,majipu nk
NAMNA YA KUITUMIA KUTIBU BAADHI YA MAGONJWA;
A.Shinikizo la damu:Tumia juisi ambayo waweza kuichanganya kwenye saladi kama chakula cha pembeni
MAANDALIZI
-Menya chengachenga za kitunguu swaumu zipatazo 10-30 na kuziponda na zikishalainika na kutoa maji kaua juisi yake na uweke kwenye chombo kisafi
-Chukua malimao 2 au 3 uyakamue upate juisi yake na ulichanganye na ile ya kitunguu swaumu na uiache usiku kucha na asubuhi koroga vizuri na anza kuitumia kwa kunywa kijiko 1 cha chai kila baada ya saa moja na hakikisha hukiachi kijiko hicho ndani ya juisi kwani hutengeneza sumu.Magonjwa ya kichwa pia hutibiwa kwa njia hii kama unataka kuitumia kutibu magonjwa kwa muda mrefu waweza kuichemsha na kuiweka katika chupa safi pindi inapopoa na utumie kikombe cha chai kila asubuhi na jioni na pia waweza kutumia saladi yake wakati wa chakula.
B.Ukurutu(fungus)-
-Twanga kitunguu swaumu na weka kwenye eneo lililoathirika na uifungie kwa bandeji na kuacha kwa nusu saa na endelea kufanya hivyo kwa muda wa wiki mbili hii ni pamoja na magonjwa ya ngozi
C.Vidonda mdomoni,mafindofindo,kuharisha,maumivu ya tumbo na kunyonga-
-Kwa matatizo mengine ya kifua kula kikonyo kimoja cha kitunguu swaumu kutwa mara tatu kulingana na ukubwa wa kitunguu.
(7)NANASI-
-Nanasi lina vitamini A,B,C pia lina madini ya chuma ,calcium, na copper ambayo ni muhimu kwenye mifupa,meno,neva na misuli(MUSCELS)
HUTIBU;
a.Matatizo mbalimbali ya tumbo,magonjwa ya bandama(SPILEN),ini,utumbo mwembamba,homa,magonjwa ya midomo(VIDONDA),magonjwa ya koo,ugonjwa wa kusahau,maradhi ya akili,hali ya kukosa mori(LOW SPIRIT)
b.Aidha nanasi huondoa matatizo ya wanawake ambayo husababishwa na upungufu wa shughuli za homoni au makosa fulani katika sehemu ya yai ,huondoa shida ya kufunga choo,baridi yabisi,upungufu wa damu(ANEMIA) na maambukizo kwenye maungio ya mifupa(ARTHRITIS).Aidha kwa kula au kunywa juisi ya nanasi husaidia akina mama wanaonyonyesha walio na maziwa kidogo na hata wale wajawazito wanashauriwa kutumia mananasi
-Pia ni kichocheo kizuri katika kupona haraka kwa mifupa iliyovunjika.
BIRINGANYA(EGGS PLANTS)-
-Tunda la biringanya ukilipika kama mboga linatibu vidonda tumbo na linasaidia kupata usingizi.Kwa wale wenye tatizo la kukosa usingizi (INSOMNIA)wanashauriwa kula biringanya kwa wingi.
-Biringanya huharakisha kupona magonjwa na kuleta afya nzuri mwilini.Ikumbukwe kuwa usingizi ni kitu muhimu sana kwa afya ya mwili wa binadamu na ustawi wake.
-Kwa kutumia tunda hili kama mboga katika mlo ulao husaidia kunenepesha kwa wale wanaotaka kunenepa.hakikisha katika mlo ulapo na ufurahie chakula unachokila kila siku ,tumia kwa muda wa mwezi mmoja utaona matokeo yake.

KWA USHAURI, MAONI,MASWALI NA TIBA TUANDIKIE KUPITIA;
lmtmherbal.blogspot.com au lmtmherbal@rocketmail.com au www.facebook.com/losila maasai au dr.elhachym.ly@gmail.com na kwa kupitia
fax2email+255736601119 


Ijumaa, 26 Aprili 2013

AINA MPYA YA KISONONO YASAMBAA DUNIANI


Aina mpya ya vimelea vya ugonjwa wa kisonono au "gono"ambavyo vinahimili dawa(resistant to drugs)zinazotumika kutibu ugonjwa huu imegundulika duniani.Taarifa iliyotolewa na shirika la afya duniani(WHO)hivi karibuni imesema,ugonjwa wa kisonono unaoathiri mamilioni ya watu ulimwenguni  umeanza kuwa sugu dhidi ya dawa zinazotumiwa kuutibu na hivyo kuna hatari ya kutoweza kutibika kabisa.Shirika la afya duniani limetoa wito kwa serikali na madaktari kuongeza ufuatiliaji wa aina hii ya kisonono kutokana na ugonjwa wa kisonono kuwa na athari nyingi kama mcharuko(inflammatoin),ugumba,matatizo wakati wa ujauzito na vifo vya akina mama wajawazito.                                                                                                                     Aina hii mpya ya vimelea vya kisonono vinaonyesha usugu wa dawa zote za antibiotiki tunazotumia dhidi yake ikiwemo dawa za jamii ya cephalosporins ambazo ni dawa za mwisho katika kutibu ugonjwa wa kisonono.Miaka michache  ijayo, aina hii mpya ya kisonono itakuwa sugu dhidi ya dawa zote ambazo zipo.Inakisiwa watu milioni 106 ulimwenguni kote huathiriwa na ugonjwa wa kisonono kila mwaka.Ugonjwa wa kisonono pia huongeza hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya ukimwi(vvu).Ugonjwa sugu wa kisonono sio tatizo la bara la ulaya au afrika pekee bali ni tatizo la dunia nzima kwa sasa,kwa mara ya kwanza vimelea sugu vya ugonjwa wa kisonono dhidi ya dawa aina ya cephalosporins viliripotiwa katika nchi ya japan ikifuatiwa na uingereza,hongkong na norway.                                                                           Wanasayansi wanaamini matumizi mabaya ya dawa aina ya antibiotiki pamoja na uwezo wa vimelea vya ugonjwa wa kisonono kubadilika na kuzoea mazingira mapya ndio chanzo kikuu cha kutokea kwa ugonjwa sugu wa kisonono na hivyo muda si mrefu ugonjwa huu utakuwa janga kubwa dunia nzima kama hatua za haraka hazitachukuliwa.Kuna uwezekano wa vimelea hivi sugu vya kisonono vinasambaa kwa sasa duniani bila kuweza kugundulika kutokana na nchi nyingi kutokuwa na utunzaji wa kumbukumbu nzuri wa ugonjwa wake.                                                                                                                                                                       Katika kituo chetu cha LMTM CENTRE tunazo dawa za LMTM/N7/SUZ ambazo zina uwezo mkubwa sana wa kutibu magonjwa yote ya zinaa (STD)sexual transmitted diseases).Kama muathirika atazitumia kwa kufuata maelekezo ya daktari na kwa dozi kamili dawa hii hutibu 100%.                                                       TOFAUTI YA KISONONO NA KASWENDE                                                                                                           Ni muhimu kueleza tofauti ya ugonjwa wa kaswende na kisonono kwa sababu kumekuwa na idadi kubwa ya wagonjwa ambao wanapotoa maelezo au malalamiko yao wamekuwa wakichanganya ugonjwa wa kaswende na kisonono.Kwa kawaida daktari anatakiwa amsikilize mgonjwa anavyojieleza kuhusu anavyojiskia kwa wakati huo,alianza kuumwa vipi na magonjwa mengine aliyowahi kuumwa hapo nyuma.Maelezo hayo kutoka kwa mgonjwa na majibu mengine atakayojibu baada ya kuhojiwa na daktari humsaidia daktari kujua vipimo vya aina gani akufanyie ili aweze kuelewa una ugonjwa gani na uko katika hatua gani ili kukupa matibabu yanayostahili.Inapotokea mgonjwa akatoa maelezo ambayo si sahihi inaweza kumfanya daktari atoe matibabu ya ugonjwa tofauti na ule unaoumwa na matokeo yake ni kuendelea kuumwa na kusababisha usugu wa ugonjwa kwa baadhi ya dawa.                                                                                               Kisonono ni ugonjwa tofauti na kaswende kwa njia mbalimbali kama ifuatavyo;kwanza kabisa tofauti kubwa ni dalili za magonjwa haya,kisonono kina dalili ya kutokwa usaha sehemu za siri ambao huambatana na maumivu makali sana wakati wa kukojoa kwa wanaume na wanawake husikia mkojo kuchoma sana wakati wa kukojoa.Kwa watoto wanaozaliwa na mama mwenye ugonjwa wa kisonono mtoto atazaliwa na ugonjwa wa macho kwa kutokwa na matongotongo mengi na macho kuwa mekundu kwa sababu ya kushambuliwa na bakteria wa kisonono.Ukweli kisonono hutambulika mapema kuliko kaswende kwa sababu dalili zake ni bayana na zinamlazimisha mgonjwa kwenda hospitali au kununua dawa za kutuliza maumivu.Kaswende ni tofauti na kisonono dalili zake ni za kuota vipele mwilini na hata uambukizaji wake ni zaidi ya kisonono,japo magonjwa yote yanaweza kuanbukuzwa kwa njia ya kujamiiana.Kaswende inaweza kuambukuzwa kwa kugusa majimaji yanayotoka kwenye vipele vya mgonjwa wa kaswende,hata kuchangia taulo au shuka na mgonjwa huyo unaweza kupata maradhi hayo iwapo majimaji yanayotoka kwenye vipele hivyo,vimegusa ngozi yako.Wadudu wa kaswende wanaweza kupenya katika ngozi ya kawaida tofauti na ugonjwa wa ukimwi ambayo yanahitaji kuwepo michubuko ili yaingie mwilini. Dalili za kaswende ni hatari sana kwani ugonjwa zaidi ya vipele huendelea kukua ndani kwa ndani bila kujua na dalili kubwa zinajitokeza wakati ugonjwa umefikia hatua ya juu zaidi.                                                                                                             Dalili hizi ni pamoja na kuongezeka kwa vipele sehemu za siri na mwili mzima,kwa kina mama mimba hutoka mara kwa mara na kwa wale watakaojifungua salama basi utakuta mtoto ana kasoro za maumbile.Kaswende imeishawafanya wengi kuishia kuwa vichaa na kuokota makopo barabarani.Hata hivyo njia za kuyaepuka magonjwa haya zinafanana sana;kuacha kufanya ngono ni bora kuliko kupata magonjwa haya mawili,hii itakusaidia kuwa na nafasi ya kujipanga na kutafuta mpenzi au mchumba na wakati utakapofika mnakubaliana maisha ya pamoja na kuwa na mahusiano  ya ngono yaliyo salama.Kuwa na mpenzi mwaminifu ni muhimu sana kama wote mtatunziana heshima na asiingizwe mtu wa tatu katika mahusiano yenu ya kingono basi ujue kuwa magonjwa hayo mtayasikia kwa wengine kwani nyie mkiwa salama itaendelea hivyo maisha yenu yote.Mwisho nawasisitiza matumizi sahihi na ya mara kwa mara ya mpira wa baba au mama maarufu kama kondomu,hii imewasaidia wengi sana.Kondomu zinazuia magonjwa ya zinaa na hata mimba zisizotarajiwa,hivyo basi tujitahidi kuuliza na kuzijua dalili za magonjwa mbalimbali ili tusiwachanganye madaktari wanapotuhudumia.                                                                                            Kwa maelekezo zaidi au ufafanuzi tuwasi                                                                                                    FAX2EMAIL +255736601119,                                                                                                                 lmtmherbal.blogspot.com                                                                                                                             EMAIL:lmtmherbal@rocketmail.com na www.facebook.com/losila maasai

Jumapili, 21 Aprili 2013

ZIJUE BAADHI YA TIBA ZA KIMASAI , MAANDALIZI NA BAADHI YA MIMEA KWA LUGHA YA KIMASAI NA KISAYANSI(BOTANICAL NAMES)-

Wamasai hasa wanaoishi milimani hutumia vitu mbalimbali katika kupambana na maradhi mbalimbali.Mara nyingi tiba hutolewa kulingana na aina ya ugonjwa,umri wa mgonjwa na mgonjwa yuko katika hali gani.Katika jamii ya kimasai tiba hufanywa na wataalam waliobobea katika tiba wanaojulikana kwa majina ya ILOIBONOK.Wataalam hawa wana heshimika sana katika jamii lakini heshima yao hupotea pale ambapo hutoa huduma kwa hisani au kwa sadaka ndogo hutoza pesa ili waweze kutimiza majukumu mengine kulingana na mahitaji yao.Katika jamii ya sasa,jamii imechangia kwa kiasi fulani kuharibu hadhi ya ILOIBONOK kwa kutowapa huduma za kutosha kulingana na umuhimu wao katika jamii husika.Kwa msingi huo wa OLOIBINI ale nini,avae nini,na afurahi vipi iwapo anao wahudumia hawasaidii kukidhi haja zake?Maswali haya humpa haki ya kutoza gharama kiasi kwaajili ya utowaji wake huduma.Muhimu ni azingatie kuwa tiba ni haki ya kila mtu hivyo aweke gharama ambayo haimfanyi tajiri kupata na masikini kukosa.                                                                                                                                                       Pamoja na kuwa kwa kipindi hiki kuna LOIBONOK wa uongo ni jukumu la jamii kuwakataa waongo ili hadhi na heshima ya LOIBONOK isidhalilishwe.Kwa hali hiyo utaalam,maarifa na ujuzi uhifadhiwe ili jamii ya maasai ihifadhike kiafya.Afya njema huwezesha jamii kuhifadhi mimea na wanyama sio kwa chakula tu bali pia kwa matibabu ya vizazi vya leo na vya baadae.Utamaduni wa kulinda kutunza na kustawisha utaimarisha na kudumisha urithi walioturithisha mababu zetu nasi tuirithishe jamii.Ikumbukwe kuwa kutunza madawa haya na kuyaenzi utaimarisha nia ya kutunza mazingira,wanyama na mimea ya asili.                                                           Kama ilivyo kichwa cha habari hapo juu,sasa tuangalie baadhi ya tiba za maasai zinavyotolewa kwa njia mbalimbali na vitu mbalimbali.                                                                                                                                        (1)KUTAFUNA-Njia hii hutumika katika utoaji wa huduma za dharura na haraka kwa kutumia miti shamba katika jamii ya maa.Majani hutafunwa na mtu asiyekuwa na vidonda kinywani na ni lazima awe mtaalam au vilevile asiwe mtaalam lakini kwa kufuata maelekezo ya mtaalam na hupakwa au kubandikwa kwenye jeraha au kukamuliwa maji yake ambayo ni mchanganyiko wa dawa na mate na kupewa mgonjwa mahututi au mtoto mdogo mgonjwa ambaye hawezi kutafuna dawa kwa uoga au udogo wake.Njia hii pia hutumika kuandaa dawa kwa ajili ya kusafisha chuchu za mama aliyetoka kujifungua muda mfupi kabla ya mtoto kunyonyeshwa.Njia hii ya kuandaa dawa za haraka kwa ajili ya kuumwa na nyoka,masikio kuuma,macho kuwasha na kuzuia kuvuja damu baada ya tohara au ng'ombe kutolewa damu kwa matumizi bila kuua ng'ombe,mbuzi au ngamia                                                                                                                                                     (2)KUKAANGA AU KUPASHA MOTO-Baadhi ya madawa huandaliwa kwa njia ya kukaanga au kupasha moto kabla haijatumika kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali,baadhi ya magonjwa hayo ni kama;vidonda vya nje,uvimbe wa matezi ,kuteguka,maumivu ya mgongo,kifua na maradhi sugu ambayo mara nyingi tiba zake hutolewa kwa kuchanganya zaidi ya aina tano za dawa ili kupata dawa iliyo bora kuliko mchanganyiko wa vitu viwili au vitatu hasa kwa magonjwa sugu nk.                                                                        BAADHI YA JAMII YA MIMEA MUHIMU KATIKA TIBA ZA MAA                                                                 (1)ILOODWA/OSEKETETI(MYSINE AFRICANA)-                                                                                                            Mti huu ni mti muhimu sana na ni dawa mama katika tiba yajamii ya maa.Kila sehemu ya mti huu ni dawa inayotibu maradhi mbalimbali ya asili na ya kisasa.Dawa hutolewa kulingana na ugonjwa unaoutibu,pia dawa hii huchanganywa na miti mingine kutegemeana na ugonjwa unaotaka kuutibu.Mchanganyiko huo hufanywa kulingana na maelekezo ya mtaalamu wa miti dawa.Baadhi ya magonjwa yanayo tibiwa kwa kutumia mti huu(oloodwai)ni;minyoo ya tumboni,tegu,minyoo uzi,maumivu ya kifua,baridi yabisi,viungo kukakamaa,kufunga choo,amoeba,typhoid,malaria,udhaifu wa mwili,kaswende,kisonono,matatizo ya ini,moyo kujaa maji,unene usio hitajika,kisukari,uchafu katika damu,vidonda vibichi,vidonda kooni,pepo punda,upungufu wa madini joto mwilini,upele,presha,fangasi nk.                                                                                                (2)ORKUJUK(PRUNUS AFRICANA)-                                                                                                                  Huu ni mti muhimu sana kwa maasai waishio sehemu za miinuko ambao hutumika kutibu magonjwa yafuatayo;homa,homa za vipindi,maumivu ya tumbo,maumivu ya mifupa,kuvimbiwa,mwili kujaa maji,miguu kuvimba,baridi yabisi,kukosa hamu ya kula,kuimarisha mifupa iliyo zeeka,malaria,bandama,kutoa sumu ya chakula,kuhara na kuhara damu nk.                                                                                                                           (3)ORKINYEI(EUCLEA DIVINORUM)-                                                                                                                   Mti huu kama ilivyo mingine ni muhimu katika tiba ya kupambana na maradhi mbalimbali katika jamii ya maa.baadhi ya magonjwa yanayotibiwa na mti huo ni;chango la mwezi,pneumonium,maumivu ya kifua,pumu,kifaduro,tambazi,uvimbe tumboni,kuharisha,minyoo,mwili kulegea,kukosa hamu ya kula na kuongeza cd4 kwa wenye vvu ikichanganywa na miti mingine kwa maelekezo ya mtaalam.                                            (4)OLNG'ERIANTUS LOO NDOYE(GALIUM APARINOIDES)-                                                                       Mti huu hutumika kutibu magonjwa yafuatayo katika jamii ya maa.Magonjwa hayo ni;mwili kuvimba,maumivu ya viungo,maumivu ya tumbo,upungufu wa madini joto,saratani,upele,kuwashwa na mwili,mapunye,unene usiohitajika,mafuta kwenye mishipa,uzito wa viungo na misuli.Kwa matokeo bora huchanganywa na miti mingine kwa ushauri wa daktari.                                                                                 MVULE/MILICIA EXCEISA-                                                                                                                                   Mti huu hutumika kusafisha damu na pia waweza kutumia kutibu magonjwa mengine kwa kuchanganya na miti mingine kulingana na ugonjwa unaoutibu.                                                                                                              (5)ORBUKOI/MKUNDEKUNDE/MLUNDALUNDA/MZOKA(CASSIA ABREVIATA)-                                Hutumika kwa kusafisha damu,hedhi kuvurugika,magonjwa ya zinaa,malaria na ugumba.                                          (6)OSENGWAI/MKUNDEKUNDE(CASSIA ALATA) -                                                                                        Hutibu minyoo,magonjwa ya ngozi,malaria,maumivu ya viungo nk.                                                                                   (7)OLOISUKI/MLUNGULUNGU/MJAFARI(ZANTHOXYLUM CHALYBEUM)-                                                  Hutibu malaria,homa,kichwa,kisukari,ngozi,hedhi kuvurugika,maumivu ya kifua,meno,fizi kutoa damu na tambazi.                                                                                                                                                                                                                   (8)OLDULE(RICINUS COMMUNIS)                                                                                                                  Huu ni kati ya miti muhimu katika tiba za asili za jamii ya maa.Baadhi ya magonjwa yanayotibiwa kwa kutumia mti huu ni;kuhamisha majipu ikichanganywa na oloisuki,kukosa hamu ya kula,kusafisha tumbo,vidonda tumbo,kuhara,kuchelewa kuzaa au kuchelewa kutoa kondo la nyuma baada ya kujifungua,pumu kwa kuchanganywa na magadi,masikio kuvuja usaha,kifaduro,kufungua tumbo lililofunga choo na kulainisha ngozi.                                                                                                                                             (9)ENDISIA(CONYTZA PYRRHOPPA)-                                                                                                                Pia ni moja ya miti muhimu katika tiba asili na tiba mbadala katika jamii ya maa inayoishi katika sehemu za miinuko.Nayo hutumika kutibu baadhi ya magonjwa yafuatayo;mafindofindo,kansa ya koo,mafua yasiyopona,mafua ya vipindi,kuvimbiwa,malaria,tumbo lililofunga choo,kusafisha figo,sumu ya chakula,mapele ya tumboni,kusafisha maziwa ya mama nk.                                                                           (10)OLMERAA(CATHA EDULIS)-                                                                                                                                 Hutumika kama kiburudisho kwa baadhi ya watu hasa vijana kwa kutafuna,hutibu kikohozi,malaria,maumivu ya mwili,kisonono,kuwashwa sehemu za siri na mafua yasiyopona.                                                                               (11)OLASESIAI(OSYRIS ABYSSINICA)-                                                                                                                              Mmea huu hupatikana katika sehemu za miinuko na hutumiwa sana kutibu baadhi ya magonjwa yafuatayo;kisonono,kaswende,matatizo ya figo,kufunga choo,kichocho,perpes,ugumba,maumivu ya hedhi,homa,matatizo ya ini,bawasiri,kuhara damu na amoeba nk.                                                                                                            (12)OSITETI(GREWUA BUCIKIR)-                                                                                                                                                                                                      Hutibu maumivu ya kifua,kuumwa na nyoka,mafua yasiyopona,maumivu ya tumbo,sumu ya chakula nk.         NB(1).Hii ni sehemu ndogo ya miti muhimu na vitu mbalimbali inayo tumika katika tiba ya jamii ya maasai.Tumeona pia jinsi baadhi ya magonjwa ya haraka yanavyotibiwa kwa kupitia wataalam wa tiba katika jami ya maa.Tutaendelea kukuletea mimea mingine na vitu vingine inayotumiwa na wamasai katika kupambana na maradhi mbalimbali katika machapisho yatakayofuata.                                                                                        (2)Madawa haya huandaliwa na kutumiwa kulingana na ugonjwa unaotaka kuutibu  na kwa wakati gani.                  Kwa maoni,ushauri na tiba tuwasiliane kupitia;                                                                                                                     LMTM CENTRE;                                                                                                                                                                           BOX.79289,DAR ES SALAAM                                                                                                                                                                                                                                              FAX2EMAIL0736601119,                                                                                                                                             EMAIL:lmtmherbal@rocketmail.com na www.facebook.com/losila maasai                                    

Ijumaa, 19 Aprili 2013

LMTM/J/19 NI DAWA BORA YA MITISHAMBA KWA VIDONDA TUMBO

Kama zilivyo jamii zingine,jamii ya kimasai ni mojawapo ya jamii inayohusika na kutibu  ugonjwa wa vidonda tumbo.Katika jamii hii ya kimasai hasa kuhusu suala la utaalam wa magonjwa na madawa yanayotumiwa kuyazuia au kuyatibu,mimea ya dawa kwa ajili ya tiba hutofautiana kulingana na jamii ya mimea,ugonjwa na ugonjwa,sehemu na sehemu,mtaalam na mtaalamu mwingine na kati ya mtu na mtu katika jamii ya kimasai.Pamoja na hayo kuna kufanana kwingi katika matumizi ya mimea sehemu za wanyama,udongo,wadudu,mikojo nk.Kutokana na kuingiliana kwa kuchanganyika na makabila mengine na uingiaji wa elimu ya kisasa ujuzi na maarifa kuhusu magonjwa na madawa umeongezeka katika jamii ya kimasai.Wamasai kwa kuishi mahali pamoja wameongeza maarifa juu ya umuhimu wa kuhifadhi mimea ili isitoweke kwa uoto wa asili kuondolewa ili kuwezesha kilimo au makazi kujengwa.Hivyo ni jambo la kawaida kukuta mimea kandokando ya boma la mmasai aliyetuama ikiwa imeoteshwa au kuhifadhiwa kwa ajili ya madawa ya watu na mifugo tu na sio kwa shughuli nyingine.                                                                                      Kwasababu hiyo katika kituo chetu cha LMTM CENTRE kwa kuegemea zaidi tiba ya miti yenye asili ya kimasai tumeamua kufanya utafiti tukishirikiana na wataalam wengine mbalimbali kubaini dawa ya kutibu vidonda tumbo.Katika utafiti wetu tumegundua dawa iitwayo LMTM/J/19 ambayo ni mchanganyiko wa mimea isiyo na madhara yenye uwezo wa kutibu kwa uhakika na kwa haraka vidonda tumbo.LMTM/J/19 mbali na kutibu vidonda tumbo kwa uhakika ina uwezo wa kutibu magonjwa mengine mbalimbali  kulingana na ugonjwa na kwa maelekezo ya daktari.Baadhi ya magonjwa hayo ni,vidonda vya njia ya chakula,ukurutu,hemorrhoids,fibroids,bawasir,maumivu ya tumbo chini ya kitovu,matatizo ya uzazi,ini,bandama,moyo kujaa maji,minyoo,maumivu ya viungo,tumbo kufunga choo,kuondoa sumu mwilini,magonjwa ya zinaa,kusafisha kibofu,kuondoa maumivu ya hedhi,misuli kukakamaa,maumivu ya mifupa,magonjwa nyemelezi kwa wenye vvu na kuongeza CD4,kuondoa mafuta kwenye mishipa ya damu,figo,kibofu,kansa ya koo,ganzi,nk.                                                                                                                                  NB:Dawa hii hutumiwa kulingana na ugonjwa unaotaka kuutibu na kwa ushauri wa daktari.                           VIDONDA TUMBO(PEPTIC ULCER)NI NINI;                                                                                                                                Ni vidonda ambavyo hutokea katika mfumo wa chakula(GASTRO INTESTINAL TRACT)ambapo huamshwa na hali ya tindikali iliyoko tumboni na huwa na maumivu makali.Hii inatokea kutokana na tabaka la ndani ya tumbo ambalo ni laini linaloteleza kumomonyoka (MUCOSAL ERROSION)na kutengeneza kishimo katika tumbo au utumbo ambacho ni kidonda.Asilimia sabini hadi tisini ya vidonda husababishwa na maambukizi ya bakteria aina ya HELICOBACTER PYLORI.Aina hii ya bakteria ni aina pekee ambao wanauwezo wa kuishi katika tindikali tumboni.Hali hii huchochewa na matumizi ya madawa yenye asili ya tindikali na sulpha.Katika mfumo wa chakula ugonjwa hushambulia sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo(DUEDENUM)ambayo ipo baada ya tumbo la chakula.Mara nyingi vidonda ambavyo vipo katika tumbo la chakula(STOMACH ULCERS au GASTRIC ULCERS)huishia kuwa saratani(MILIGANT TUMOUR).                                                                                                                                                                 Ugonjwa huu huwasumbua wakubwa na wadogo,wanaume na wanawake na ni hatari sana kutokana na madhara yake.Ni mara chache sana kuupata kutokana na maambukizi.Walio wengi huupata kutokana na mabadiliko katika mfumo wa maisha kama ulaji na unjwaji mbovu.                                                               Ugonjwa huu umegawanyika kutokana na sehemu iliyoathirika kama ifuatavyo:                                             (a)DOUDENAL ULCERS-Hapa ugonjwa huanzia katika sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo(DOUDENUM)                                                                                                                               (b)OESOPHAGAL ULCERS-Hapa ugonjwa utakuwa katika njia ya kushukia chakula(OESOPHAGAS)   (c)GASTRIC ALCERS-Hapa ugonjwa unakuwa katika tumbo la chakula                                                                         (d)MECKEIS DIVARTICULUM ULCERS-Ukiwa katika tumbo ambapo huambatana na maumivu makali endapo mgonjwa ataguswa tumbo.                                                                                                                                DALILI ZA VIDONDA TUMBO;                                                                                                             (a)Maumivu ya tumbo-Maumivu haya huanza katika chembe ya moyo(EPIGASTRIC PAIN)na huwa makali masaa mawili hadi matatu baada ya kula.(DUEDENAL ULCERS).Endapo maumivu haya ya tumbo yanakuwepo na kuwa makali kabla ya kula yaani yanakuwepo wakati una njaa na kutulia baada ya kula hapo ni GASTRIC ULCERS ambayo mara nyingi huishia kuwa saratani(MALIGNANT TUMOUR)             (b)Tumbo kujaa(BLOATING/ABDOMINAL GASTRITIS/ACIDIOSIS)-Katika hali hii mgonjwa huhisi kujaa gesi tumboni ,kuhisi kichefuchefu na hata kutapika,kukosa hamu ya kula,kiungulia,kucheua mara kwa mara,mate kuwa machungu,kupungua uzito na kufunga choo au kupata kikiwa kigumu kama cha mbuzi.                    (c)Kutapika damu(MEHA TEMESIS)-Hii hutokea endapo damu itatoka moja kwa moja kwenye kidonda hali ambayo huwapata wenye GASTRIC na OESOPHAGAS ULCERS au wale wanaotapika mara kwa mara                                                                                                                                                                                (d)Kupata choo cheusi(MELENA)-Mgonjwa hupata choo cheusi kama lami na hutoa harufu kali kutokana na damu kutoka ndani katika sehemu ya utumbo mdogo ambako kwa wenye historia ya kiungulia mara kwa mara na kuhisi moto kifuani na akitumia magnesium,tagament,omaprazole,tapha au cenetidimine huisha,basi ni dalili za mwanzo za kupatwa na vidonda tumbo.                                                                                                            Katika kituo chetu cha LOSILA MAASAI TRADITIONAL MEDICINE (LMTM)mbali na dawa tuliyoitaja hapo juu(LMTM/J/19)ambayo ni tiba sahihi kwa vidonda tumbo tunatoa pia tiba za vidonda tumbo kwa kutumia mimea kama mbogamboga,matunda,na ushauri wa namna mgonjwa wa ugonjwa wa vidonda tumbo atakavyoishi kwa mfano;chakula,vinywaji,matunda,n.k.Tunatibu pia magonjwa yanayoambatana na ugonjwa wa vidonda tumbo(nguvu za kiume na saratani(MILIGANT TUMOUR)).                        Msisitizo;Dozi ya dawa hii hutolewa kulingana na ugonjwa,uzito na umri kulingana na maelekezo ya daktari na pia hutumiwa na mtu yeyote(mama mjamzito au anayenyonyesha)bila madhara yoyote.                                     Kwa maoni,tiba,ushauri wasiliana na;                                                                                                                          LMTM;                                                                                                                                                                      BOX 79289,DAR ES SALAAM                                                                              FAX2EMAIL0736601119                                                                                                                                       EMAIL;lmtmherbal@rocketmail.com na www.lmtm.blogspot.com