Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 6 Julai 2014

ZIJUE DALILI,TIBA NA UCHUNGUZI WA TATIZO LA MAWE KWENYE FIGO







      TATIZO LA MAWE KWENYE FIGO(KIDNEY STONES)
-Figo ni kiungo muhimu katika mwili wa binadamu,hufanya kazi ya kuchuja damu huku ikiondoa sumu zote za mwili,figo hufanya kazi ya kurekebisha kiasi cha maji mwilini(electrolyte level).
kabla damu haijapita katika figo,huwa imebeba maji na takataka nyingi sana(urea),lakini inapopita katika figo huchujwa na vitu muhimu hurudishwa katika mzunguko wa damu lakini,masalia mengine ambayo hayafai tena katika mwili ikiwa ni pamoja na kiwango cha maji kilichozidi hupitishwa kwenye mirija miwili(ureters)kuelekea kwenye kibofu(urinary bladder) na kishas kutolewa nje ya mwili kupitia njia ya mkojo(urethra)
Mkusanyiko wa kemikali hizi(chemical crystals),wakati mwingine hugandamana na kutengeneza chembechembe ya vitu kama mchanga,kadri siku zinavyozidi kuendelea ndivyo vinavyozidi kukua hadi wengine hufikia hatua ya kuziba njia ya mkojo katika figo yenyewe(neprone) au kwenye mirija ya kupeleka mkojo kutoka kwenye figo kwenda kwenye kibofu(ureteter),hapo ndipo mtu anaanza kupata shida ya kukojoa na kusikia maumivu makali.


     DALILI ZA UWEPO WA MAWE KWENYE FIGO;
  Mtu mwenye mawe kwenye figo huonyesha dalili zifuatazo;
a.Maumivu ya mgongo na kiuno
b.Mkojo kutoka ukiwa na rangi ya damu
c.Kutokwa na jasho wakati wa usiku
d.Kupatwa na homa kali kwa wakati flani ikiambatana na kutetemeka mwili
e.Kuhisi kichefuchefu na kutapika
f.Mkojo kuwa na harufu kali
g.Maumivu makali sehemu za mbavu
h.Miguu kujaa maji/kuvimba.
i.Maumivu ya tumbo chini ya kitovu upande wa kushoto au kulia kutegemea ni figo ya upande gani iliyoathirika.
j.Maumivu makali unapogusa upande wa figo iliyoathirika.

   KISABABISHI CHA MAWE KATIKA FIGO(KIDNEY STONES);
1.Matumizi ya baadhi ya dawa husababisha mtu kupata mawe katika figo pindi anapozitumia kila mara.Dawa hizo ni kama vile za kutibu kansa na HIV,antibiotic kama ciprofloxacin,cefrtriaxone na madawa yenye sulphur kama metacalphin nk.
2.Utumiaji wa vyakula vyenye kuongeza vitamin A na D,ambavyo huongeza kwa kiasi kikubwa madini joto mwilini
3.Kuishi kwenye mazingira ya joto sana bila kupata maji ya kutosha husababisha kiasi cha chemical kuongezeka katika figo na kusababisha zigandamane na kutengeneza mawe ndani ya figo.
4.Maambukizi ya magonjwa ya figo kama renal tubula acidocis ctc,huongeza hatari ya kupata tatizo hilo.
5.Kurithi kutoka kwa wazazi (wanakuwa na homoni ziitwazo antiduretic hormone)zisizoweza kufanya kazi ya kuchuja damu kikamilifu na mwishowe hutengeneza mawe katika figo.
6.Utumiaji wa vyakula vyenye protin zinazotokana na wanyama na chumvi nyingi(huongeza hatari ya kupata tatizo hili)
7.Unene kupita kiasi

   JINSI YA KUGUNDUA TATIZO;
1.Mgonjwa kufanyiwa X-Ray au scan ili kujua kama ana mawe katika figo.
2.Vipimo vya damu(blood test)
3.Vipimo vya mkojo(urenarlulisis)

    TIBA YA TATIZO;
-Ikiwa mgonjwa baada ya uchunguzi atagundulika kuwa na tatizo hili hupewa mojawapo ya tiba zifuatazo:
1.Extracorporeal shock wave lithotripys(eswl)-Hii ni mionzi inayoelekezwa katika figo ili kuyeyusha mawe (chemical au sumu zilizogandamana)ambazo huvunjwavunjwa na hii mionzi kisha mgonjwa hukojoa vipandevipande.
2.Percutaneous nephrolithotomy(PCNL)-Hiki ni kifaa chenye mwanga na kamera ambacho huingizwa kwenye kokwa za figo (nephrone)ambayo huvunjavunja mawe katika figo.
3.Ureteroscopy-Kifaa hiki huingizwa kwenye mirija ya kupitishia mkojo(urether)kutoka kwenye figo kwenda kwenye kibofu ili kuondoa mawe yaliyokwama kwenye mirija na kuzuia mkojo kutoka.
4.Stone removal-Hapa mgonjwa hufanyiwa operesheni ya kuondoa mawe moja kwa moja.

- Kama tulivyoona tiba hizi zina madhara na ni ghali.Hivyo basi kabla hujaenda katika tiba hizi zenye madhara makubwa ni muhimu kutumia tiba mbadala na tiba asili ili kuepuka madhara mengine.
Katika kituo chetu cha LMTM HERBAL CENTRE tunayo dawa asili zenye uwezo mkubwa wa kutibu tatizo hili la mawe kwenye figo bila madhara yoyote.Aina hizi za dawa hufanya kazi za kuyeyusha kemikali na mafuta yaliyogandamana katika figo na kuzibua mirija iliyojiziba ili kuruhusu mtiririko wa mkojo kuwa kama unavyotakiwa.
Baadhi ya madawa tuliyonayo ni;
a.LMTM-F5/AFH2
b.LMTM/S32/J
Dawa hizi mbali na kutibu matatizo ya mawe katika figo zinauwezo wa;
1. kutibu saratani ya kizazi,kusafisha mirija ya uzazi na kutoa maji katika mirija hiyo
2.Uvimbe wowote ndani ya mwili
3.Kurekebisha hedhi iliyovurugika kwa akina mama(hasa waliowahi kutumia dawa za uzazi wa mpango)
4.Saratani ya ini na kibofu cha mkojo
5.Kusafisha mfumo mzima wa njia ya mkojo
6.Huwasaidia akina mama wenye kasoro mbalimbali katika via vya uzazi,waotafuta uzazi kupata watoto