Tafuta katika Blogu Hii

Jumanne, 17 Septemba 2013

MAASAI TRADITIONAL MEDICINE(TIBA ASILI ZA KIMASAI): KASWENDE NI HATARI KULIKO MAGONJWA MENGINE YA ZINA...


MAASAI TRADITIONAL MEDICINE(TIBA ASILI ZA KIMASAI): KASWENDE NI HATARI KULIKO MAGONJWA MENGINE YA ZINA...: Kaswende ni ugonjwa tishio linalosababishwa na bakteria wanaofahamika kama Treponema pallidum.Tofauti na magonjwa mengine ya zinaa ambayo hu...

KASWENDE NI HATARI KULIKO MAGONJWA MENGINE YA ZINAA EG UKIMWI NK.


Kaswende ni ugonjwa tishio linalosababishwa na bakteria wanaofahamika kama Treponema pallidum.Tofauti na magonjwa mengine ya zinaa ambayo huambukizwa kwa njia ya ngono zisizo salama,kaswende ni hatari zaidi kwani inaweza kuambukizwa kwa kugusana tu au kushirikiana mavazi,kushirikiana vyoo vya kukaa japo pia waweza kuambukizwa kwa kupitia ngono zisizo salama.
Katika hatua za awali vipele sehemu za uzazi au sehemu yoyote mwilini hujitokeza muda mfupi baada ya maambukizi ambavyo baadae hupotea vyenyewe bila kutibiwa.
 Kama ugonjwa hautatibiwa maambukizi huendelea kwa miaka yakishambulia mifupa,ubongo na moyo na kusababisha madhara mengine katika mfumo wa fahamu kama vile,homa ya uti wa mgongo,magonjwa ya moyo na kiharusi.
Kaswende wakati wa ujauzito ni hatari kubwa kwa kiumbe kilicho tumboni kama vile kusababisha kutoumbika vizuri yaani deformity na kifo.

(1)Katika makala yetu ya leo tutazungumzia madhara ya kaswende katika mfumo wa mishipa ya fahamu(Neurosyphilis)

Madhara ya ugonjwa wa kaswende katika mishipa ya fahamu hutokea miaka 10-30 baada ya mtu kuugua ugonjwa wa kaswende na ambaye hakupata tiba yoyote hapo awali.Madhara haya huonekana kwenye uti wa mgongo na kwenye ubongo.
Kuna aina nne za Neurosiphilis:
1.Isiyo na dalili(Asymptomatic)-katika aina hii mgonjwa anakuwa hana dalili zozote.Aina hii ndiyo huonekana sana kwa wagonjwa ambao hawakupata tiba hapo awali.
2.Ulemavu wa jumla(General paresis)-inayosababisha ulemavu wa jumla
3.Inayoshambulia tando za ubongo na mishipa ya damu(Meningovascular)
4.Inayoshambulia sehemu za chini za uti wa mgongo(Tabes dorsalis)
-General paresis husababishwa na kuathirika kwa ubongo na hivyo kuleta upungufu katika ufanyaji kazi wa ubongo(Impairement of mental function)
Aina hii pia huweza kutokea kwa wagonjwa wa kisonono(Gonorrhoea)

Dalili za general paresis ni kama ifuatavyo;
a)Kupungua uwezo wa kuzungumza(aphasia)
b)Kupungua uwezo wa kufanya maamuzi(impaired judgment)
c)Kutokuwa na uwezo wa kuhesabu kitu chochote
d)Kupungua kuhamasika(impaired motivation)
e)Kutokuwa na kumbukumbu ya vitu vilivyopita muda mrefu(loss of long term memory)
f)Kutokuwa na kumbukumbu ya vitu vilivyopita karibuni/muda mfupi(loss of short term memory or recent events)
g)Degedege
h)Kushindwa kutembea au kutumia miguu,mikono, na viungo vingine vya mwili
i)Mabadiliko ya kitabia na kihisia(personality changes)kama delusions,kuona au kusikia vitu visivyokuwepo(hallucinations)
j)Kukasirika kwa haraka(irritability)
k)Inapropiate moods
l)Low mood

Viashiria vya general paresis;
a)Mboni za jicho kuwa katika umbile ambalo si la kawaida
b)Mboni kushindwa kupepesuka(changes in pupil response)
c)Kupoteza uwezo wa kuhisi mgandamizo au mtikisiko katika ngozi(loss of sense of vibration or position)
d)Kushindwa kusimama wakati mtu amefunga macho(romberg test)
e)Kushindwa kutembea vizuri
f)Viungo vya mwili kuwa dhoofu
g)Matatizo ya kusahau.
-Dalili za meningovascular
a)Mboni kuwa ndogo
b)Kupooza kutokana na kuathirika kwa neva mbalimbali
c)Kuharibika mishipa ya damu mwilini
d)Kupooza upande mmoja wa mwili
e)Matatizo ya kumeza chakula
f)Degedege
g)Kupooza neva ya jicho(optic neuropathy)
h)Matatizo ya macho(chorioretinitis)
i)Uziwi
j)Vertigo


-Dalili za tabes dorsalis
a)Kutembea kwa shida
b)Mgonjwa kutembea huku ametanua miguu sana(wide based gait)
c)Kudhoofika viungo vya mwili
d)Kupoteza uwezo wa kuunganisha hisia na matendo fulani fulani katika mwili(loss of coordination)
e)Kuwa na hisia zisizo za kawaida mwilini kama vile;kujihisi vitu vinachomachoma(lightening pains)
f)Loss of reflexes

-Tiba ya Neurosyphlis;
Tiba ya aina zote nne za neurosyphlis huhusisha kwanza kutibu ugonjwa wa kaswende kwa kutumia dawa.Sisi LMTM CENTRE tunayo dawa inayotibu magonjwa yote sugu ya zinaa ikiwemo kaswende inayoshambulia mishipa ya fahamu iitwayo LMTM-N7/SUZ ambayo ni mchanganyiko wa miti isiyo na madhara yoyote kwa mtumiaji.Dawa hii ni ya kunywa kulingana na uzito na hali ya ugonjwa kwa ushauri wa daktari.
Kwa wale wagonjwa wasioweza kula,kuvaa nguo,waliopooza viungo,wasioweza kuzungumza watahitaji tiba mbalimbali kama;rehabilitation therapy,physical therapy,occupation therapy,speech therapy n.k.Kwa wale viziwi watahitaji vifaa maalum vya kuwasaisaidia kusikia (hearing aids)baada ya kuonana na daktari wa masikio,pua na koo.

Kumbuka kuwa ili kugundua aina ya ugonjwa ulionao ni lazima upate vipimo sahihi kulingana na ni ugonjwa gani unaotaka kuupima.Vipimo hivi hupatikana katika hospitali za rufaa na kwa ushauri na maelekezo ya daktari baada ya kupata historia fupi ya mgonjwa.Ikumbukwe kuwa ugonjwa wa kaswende umekuwa janga la kimataifa kwa kuwa sugu kwa madawa yaliyokuwa yakitumika kutibia hapo awali sawasawa na kisonono zote kwa sasa hazisikii dawa.Ni LMTM HERBAL CENTRE pekee yenye uwezo wa kuyatibu.

MAONI,USHAURI,TIBA TUWASILIANE;
fax2email+255736601119
PIA USIACHE KULIKE PAGE YETU YA LMTM HERBAL CENTRE